"CHADEMA haina uwezo wa kushika Dola Kutokana na Mfumo wake wa utawala kuwa mbovu unaotokana na udikteta, udini na ukabila ".... Asema Elizabeth Minde



Chama  cha  mapinduzi  ( CCM)  manispaa  ya  Moshi  mkoani  Kilimanjaro   kimeendelea  kusisitiza  kuwa  chama  cha  demokrasia  na  maendeleo, CHADEMA   hakitaweza  kushika  dola  kutokana  na  mfumo  wake  wa  utawala  kuwa  mbovu....

Kauli  hiyo  ilitolewa  jana  na  mwenyekiti  wa  CCM manispaa  ya  Moshi, Elizabeth Minde  wakati  alipokuwa  akimnada  mgombea  wa  udiwani  wa  kata  ya  Kiboriloni  kwa  tiketi  ya  chama  hicho, Willy Adriano...

Mwenyekiti  huyo  alisema  migogoro  inayoendelea  ndani  ya  chama  hicho  ni  ishara  ya  utawala  mbovu  unaotokana  na  udikteta, udini  na  ukabila, hivyo  chama  hicho  kupewa  dola  ni  kuhatarisha  amani  ya  nchi  hii  ambayo  imekuwa  nembo  ya  taifa  hili  kimataifa...

Alisema  CCM imejipanga  vya  kutosha  kupata  ushindi  katika  uchaguzi  huo  huku  akiwatahadharisha  wanaoibeza  CCM  kuwa  tayari  kuingia  aibu  ufikapo  februari 9  maka  huu...

"Ili  mwananchi  aweze  kupata  maendeleo  tunahitaji  kupata  kiongozi  makini  ambaye  ataweza  kuwaletea  wananchi  maendeleo, hivyo  nawaomba  wananchi  wa  kata  ya  Kiboriloni  wamchague  Willy Adriano, CCM ushindi  unakuja"..Alisema  Minde

Kwa  upande  wake  katibu  mwenezi  wa  CCM mkoa, Michael  Mwita, alisema  kazi  ya  CCM ni  kuisimamia  serikali  katika  kutekeleza  shughuli  za  kimaendeleo  kutokana  na  ilani  ya  chama  hicho.

"Asilimia  90  ya  wakazi  wa  Kiboriloni  wanakabiliwa  na  changamoto  lukuki, huwezi  kuwa  na  mbunge  ambaye  ana  maslahi  yakwake.Kuna  wapanda  mlima  wamekuwa  wakinyanyasika  na  malipo  yao  duni, lakini  imekuwa  ngumu  kwa  mbunge  huyo  kuwatetea  vijana  hao" Alisema  Mwita

Aliongeza  kuwa  mbunge  huyo  tangu  achaguliwe  mwaka  2000  hakuna  maendeleo  yoyote  aliyowaletea  wananchi  wa  Moshi  pamoja  na  kutoa  ahadi  lukuki  ikiwemo  ahadi  ya  kurudisha  soko  la  Kiboriloni  ambalo  kwa  sasa  limehamishwa.

Alisema  mbunge  huyo  hana  nia  ya  dhati  ya  kuwakomboa  wananchi  wake  tofauti  na  anavyodai  katika  majukwaa  ya  siasa  na  kuongeza  kuwa  mwaka  2010  aliwaahidi  wamachinga  kuwa  endapo  watamchagua  na  kumpa  halmashauri  atahakikisha  machinga  hawanyanyaswi  huku  akiahidi  kuwajengea  machinga  complex, ahadi  ambayo  haijatekelezwa  hadi  sasa.

0 comments: